Tuesday, 5 May 2015

WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAKWAMA VITUONI ,, MGOMO WA MABASI DAR !

Wanafunzi walioanza mitihani ya Taifa ya kidato cha sita wamekuwa miongoni mwa watu walioathirika na mgomo wa madereva katika maeneo mbalimbali nchini.
 
Katika maeneo mengi jana, wanafunzi pamoja na abiria walikaa vituoni kwa muda mrefu, ingawa baadhi ya magari binafsi yalikuwa yanatoa msaada kwa baadhi yao.
Mkazi wa Songea, Nasri Isack alisema watoto wake walishindwa kuhudhuria masomo na alilazimika kukodi teksi ili mwanaye awahi shuleni kufanya mtihani wa kidato cha sita.

 
Aliongeza kuwa yeye binafsi alilazimika kukodi teksi kwenda hospitali ya Peramiho kwenye matibabu baada ya daladala kugoma.
“Hivi kwanini Serikali haitaki kumaliza hili tatizo, wanapata furaha gani kuona wananchi tunavyoteseka na huu mgomo usioisha?
“Leo nimetoa zaidi ya Sh60,000 ili kumwahisha mwanangu akafanye mtihani wa kidato cha sita, pamoja na mimi mwenyewe kwenda kutibiwa Peramiho, hii ni pesa nyingi kwangu kwani kusingekuwa na mgomo tungetumia Sh3,000 tu, nimesikitika sana,” alisema.
Jijini Mbeya makundi ya wanafunzi wakiwamo wa kidato cha sita walianza kusota barabara tangu saa 11.30 alfajiri ambapo daladala hazikuonekana ingawa bajaji na pikipiki zilikuwa zikifanya kazi wakati huo.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Sangu, Andongwisye Bukuku aliliambia gazeti hili kwamba baadhi ya wanafunzi wake hususani wa kidato cha sita walioanza mitihani yao ya mwisho waliathirika na mgomo huo.

No comments:

Post a Comment