Barack Obama na Benjamin Netanyahu wote wawili waliingia
madarakani mwaka 2009 na kati yao uhusiano umedorora. Katika hotuba yake
mjini Cairo mwaka huo, Rais wa Marekani kwa alitangaza akisisitiza
kwamba ukoloni wa Israel kwenye maeneo ya Palestina unapaswa kusitishwa.
Akizungumza Jumatatu wiki hii na Waisraeli wenye uraia wa Marekani, Netanyahu alisema anaiheshimu serikali ya Obama na kusisitiza kuwa Marekani na Israeli haziungi mkono mradi wa Nyuklia nchini Iran lakini wao kama viongozi wanatofautiana kuhusu njia gani ya kutumia ili kuizuia Iran kuendelea na mradi huo.
Naye Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry akizungumza akiwa jijini Geneva nchini Uswizi amemtaka Netanyahu kutogusia yale waliyokubaliana na Iran kuhusu mradi wake, hali ambayo inaweza kusababisha mazungumzo kukwama.
Israel imesema, mpango wa Nyuklia wa Iran unaendelea kutishia usalama wa Israel.
Akizungumza Jumatatu wiki hii na Waisraeli wenye uraia wa Marekani, Netanyahu alisema anaiheshimu serikali ya Obama na kusisitiza kuwa Marekani na Israeli haziungi mkono mradi wa Nyuklia nchini Iran lakini wao kama viongozi wanatofautiana kuhusu njia gani ya kutumia ili kuizuia Iran kuendelea na mradi huo.
Naye Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry akizungumza akiwa jijini Geneva nchini Uswizi amemtaka Netanyahu kutogusia yale waliyokubaliana na Iran kuhusu mradi wake, hali ambayo inaweza kusababisha mazungumzo kukwama.
Israel imesema, mpango wa Nyuklia wa Iran unaendelea kutishia usalama wa Israel.
No comments:
Post a Comment