Takriban watu 175 wamefariki kufiakia sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.
Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha raia wengi bila makaazi pamoja na stima.
Tarayi Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
Rais wa Ghana,John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena.
No comments:
Post a Comment