Historia yake
Edward Lowassa alizaliwa Agosti 26, 1953 katika
Kijiji cha Ngarash, Monduli na ndiye mtoto mkubwa wa kiume kwa Mzee
Ngoyai Lowassa (atafikisha miaka 62 Agosti mwaka huu). Alianza kusoma
katika Shule ya Msingi Monduli kati ya mwaka 1961–1967.
Kisha akaendelea kwenye Shule ya Sekondari Arusha
kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne kati ya mwaka 1968 - 1971, kabla ya
kumalizia kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Milambo
mkoani Tabora mwaka 1972–1973.
Alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka
1974–1977 na kuhitimu Shahada ya Sanaa katika Elimu (B.A Education) na
baadaye Chuo Kikuu cha Bath Uingereza kwa Shahada ya Uzamili ya Sayansi
katika Maendeleo (mwaka 1983–1984).
Baada ya kumaliza chuo kikuu, Lowassa alifanya
kazi ndani ya CCM akiwa ofisa wa ngazi ya juu kuanzia wilaya, mkoa na
baadaye makao makuu kati ya mwaka 1977–1989.
Aliajiriwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano ya Kimataifa Arusha (AICC), mwaka 1989–1990.
Lowassa amemuoa Regina na wana watoto watano,
wasichana wawili na wavulana watatu. Watoto hao ni Fredrick, Pamella,
Adda, Robert na Richard.
Mbio za ubunge
Lowassa alichaguliwa kuwa Mbunge wa Monduli mwaka
1990 na 1993 aliteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu na
Makamu wa Kwanza wa Rais (Haki na Mambo ya Bunge), kabla ya kuhamishiwa
Wizara ya Ardhi na Makazi akiwa Waziri mwaka 1993–1995.
Kwenye Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa vyama vingi
(mwaka 1995), Lowassa alishinda ubunge kwa asilimia 87.3. Alikaa bila
uteuzi wowote kwa miaka miwili. Mwaka 1997–2000, Rais Benjamin Mkapa
alimteua kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na
Kuondoa Umasikini).
Kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 aligombea tena
ubunge wa Monduli na kushinda kwa mara ya tatu. Rais Mkapa akamteua kuwa
Waziri wa Maji na Mfugo hadi mwaka 2005.
Kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2005, aligombea ubunge na
kushinda kwa asilimia 95.6. Rais Jakaya Kikwete alimteua kuwa Waziri
Mkuu wa Tanzania na Bunge likamthibitisha kwa kura 312.
Baada ya kujiuzulu, Lowassa aligombea ubunge kwa mara nyingine Monduli (mwaka 2010) na kupata asilimia 90.93 ya kura zote na hadi sasa ndiye mbunge wa jimbo hili japokuwa amekwishaaga kwamba hatagombea tena kiti hicho.
Mbio za urais
Nguvu yake
Uwaziri mkuu wa Lowassa ulikoma Februari 2008, alipojiuzulu
kutokana na kashfa ya Richmond. Kamati Maalumu ya Bunge ya watu watano
iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe ilisisitiza kuwa wizara ya Nishati
na Madini na Ofisi ya Waziri Mkuu ndizo zinazopaswa kubeba lawama ya
uingiaji wa mkataba mbovu na Richmond, kampuni ambayo uchunguzi
ulionyesha kuwa ni ya mfukoni mwa watu huku Serikali ikilazimika kulipa
mabilioni ya fedha katika mkataba ambao una upungufu makubwa.
Wakati Lowassa analitaarifu Bunge kuwa
amemuandikia Rais barua ya kujiuzulu, alisisitiza kuwa “…anafanya hivyo
ili kulinda taswira ya chama chake na Serikali na kuwa shida ya wabaya
wake ni u-waziri mkuu na siyo kingine…”
Baada ya kujiuzulu, Lowassa aligombea ubunge kwa mara nyingine Monduli (mwaka 2010) na kupata asilimia 90.93 ya kura zote na hadi sasa ndiye mbunge wa jimbo hili japokuwa amekwishaaga kwamba hatagombea tena kiti hicho.
Mbio za urais
Lowassa ni miongoni mwa wana CCM 17 waliochukua fomu kuwania urais mwaka 1995 lakini aliyepitishwa ni Mkapa.
Mwaka 2005, hakugombea urais ila alikuwa na
mipango ya muda mrefu ya kumsaidia rafiki yake, Kikwete na inadaiwa kuwa
makubaliano ya Kikwete na Lowassa yalikuwa kwamba mwenzake akishaongoza
nchi kwa miaka 10 (yaani 2005 – 2015) atamtengenezea njia 2015 – 2025.
Kabla mipango hiyo haijatimia ndipo Lowassa
akapata kile ambacho Kikwete anakiita “ajali ya kisiasa”. Lakini hata
baada ya ajali ya kisiasa kutokea, nimeambiwa walikuwa na makubaliano
mengine kuwa “Kikwete angesaidia kumsafisha rafiki yake” ili mwaka huu
2015 ufikapo aweze kumuachia Ikulu ya Magogoni.
Tangu Lowassa aachie uwaziri mkuu na tangu agundue
kuwa Kikwete ‘amemkalia” kimya, alianza juhudi zake mwenyewe za
kujitengenezea njia ya kuelekea Ikulu na amefanya mambo mengi
yanayoashiria kuwa amedhamiria kuingia Magogoni.
Kama kuna mtu nchi hii ametoa michango mingi ya
rasilimali fedha katika kuchangia misikiti, makanisa, vijana, vikundi,
harambee na vinginevyo, hakuna kama Lowassa. Michango hiyo, wachambuzi
wengi wanaihusisha na mbio zake za urais.
Nguvu yake
Nguvu ya kwanza ya Lowassa ni umaarufu, yeye ni
maarufu kuliko wagombea wote wa CCM, ndani na nje ya chama hicho. Yeye
ndiye anatajwa kuliko wenzake wote na hili halina shaka.
Nguvu ya pili ya Lowassa iko kwenye uwezo wa
kirasilimali (watu na fedha). Lowassa na mtandao wake wana rasilimali za
kutosha kuendesha harakati hizi. Kwa siasa za CCM ya miaka hii
iliyowatupa mkono wakulima na wafanyakazi, rasilimali (fedha na watu) ni
kila kitu. Jambo hili linampa nguvu zaidi dhidi ya wagombea wenzake
ambao nao wanahaha huku na kule kuzisaka.
Jambo la tatu linalompa Lowassa nguvu ni kuwahi kuwa Waziri Mkuu
na kuijua kwa undani mifumo ya uendeshaji wa nchi na hata kuisimamia.
Ushawishi wake kwa mifumo hiyo umeendelea hadi sasa na nimeambiwa kuwa
kuna taasisi muhimu za kidola zimegawanyika kwa sababu ya kumuunga
mkono, watendaji serikalini nao wamegawanyika kwa ajili yake na kila
mmoja ana hofu kuwa asipofanya “booking” kwenye kambi ya Lowassa,
anaweza kukosa vyeo bwerere kwenye Serikali ijayo.
Alipokuwa Waziri Mkuu alionyesha misimamo ya
kiuongozi na kuthubutu kwingi kunakotakiwa kufanywa na mkuu wa nchi,
lakini misimamo yake na uthabiti wake unahusishwa pia na kujikuta mara
nyingi akifanya uamuzi wenye makosa mengi au wenye kuzua maswali mengi
ya kisheria.
Lakini jambo la nne ni kuzijua njia zilizompa
madaraka Kikwete mwaka 2005. Kati ya wagombea wote wa CCM kwa sasa,
huenda ni Lowassa peke yake ndiye anayezijua vizuri njia alizotumia
Kikwete kujenga mtandao mkubwa wa ushindi mwaka 2005, makanisani,
misikitini, vyuoni na kwingineko, hadi nyumba za ibada zikaimba “Kikwete
ni chaguo la Mungu”. Kwa hiyo anajua njia ipi apite kuwashinda wagombea
wengine.
No comments:
Post a Comment