KOCHA Mkuu wa Manchester United, Louis
van Gaal, amesema sasa anaweza kupata nguvu ya kutazama mechi za
Liverpool tena akiwa na glasi ya mvinyo baada ya kushinda mabao 2-1
ugenini kwa Crystal Palace juzi Jumamosi.
Van Gaal alisema mechi hiyo ilikuwa muhimu kwao na
kama wangefungwa au kutoka sare, basi asingekuwa na uthubutu wa
kutazama mechi za Liverpool, mshindani mwenzake kwenye kusaka nafasi ya
nne katika Ligi Kuu England.
Liverpool jana Jumapili jioni ilitarajia kumenyana
na mabingwa Chelsea na Van Gaal alisema mechi hiyo haina tena presha
kwake na anatazama huku akiwa na kinywaji mkononi.
Mabao ya Juan Mata na Marouane Fellaini yalitosha
kuipa ushindi Man United na kuondoa presha ya kocha wake ambapo sasa
anatakuwa anasaka ushindi wa mechi moja tu kati ya mbili kujihakikisha
nafasi ya nne.
Kabla ya mechi ya jana ya Liverpool, Man United
iliikua imeiacha timu hiyo kwa pointi saba, pengo ambalo linamfanya
Mdachi huyo kuamini kwamba hawezi kufikiwa na Liverpool kwa mechi
zilizobaki kama watashinda mechi moja kati ya mbili walizobakiza kwenye
Ligi Kuu.
“Soka ni mchezo wa uchizi sana, hebu tazama vile
tulivyocheza dhidi ya Chelsea, Everton na West Brom tulikuwa bora
uwanjani tofauti na mechi hii ya Crystal Palace,” alisema
“Hii mechi tuliyocheza hovyo tumeshinda, zile tulizocheza vizuri
zote tumefungwa, ndivyo soka lilivyo.”
No comments:
Post a Comment