Polisi nchini Malaysia wanasema kuwa
wamepata karibu makaburi 140 na kile wanaamini kuwa ni kambi 28 haramu
za kuwasafirisha watu kimagendo karibu na mpaka na Thailand.
Mkuu wa polisi nchini Malaysia Khalid Abu Bakar, anasema wanaamini kuwa makaburi mengine yanazaidi ya maiti moja.
Aidha makaburi hayo yalitumiwa kuzika wahamiaji ambao walikufa wakiwa kizuizini. Ugunduzi kama huo ulifanyika nchini Thailand
Ugunduzi kama huo ulifanyika
nchini Thailand yapata mwezi mmoja uliopita na kutibua operesheni kali
dhidi ya walanguzi wa binadamu. Mkuu wa polisi nchini Malaysia Khalid Abu Bakar,
anasema wanaamini makaburi mengine yako na zaidi ya maiti moja
Oparesheni hiyo iliyoendeshwa
na jeshi la wanamaji na polisi wa Thailand iliwaacha maelfu ya watu
wakiwa wametelekezwa baharini ,na ikalazimu mashirika ya kupigania haki
ya kibinadamu na wakimbizi kuingilia kati ilikuzishinikiza serikali za
mataifa husika kuwaruhusu wahamiaji waliokuwa kwenye mashua hizo za
wakimbizi kuweka nanga katika bandari zao.
Operesheni hiyo ilikuwa inawalenga walanguzi wa watu wa jamii ya waislamu wa Rohingya kutoka Myanmar na Bangladesh.
Waziri
wa masuala ya ndani wa Malaysia aliviambia vyombo vya habari kuwa
ameshangazwa kugundua kuwa huenda kambi hizo zimekuwa eneo hilo kwa
miaka mitano.
No comments:
Post a Comment