Kiungo wa Real Madrid Gareth Bale
ameelezea matarajio yake ya kuendelea kubaki ndani ya klabu hiyo msimu
ujao, japokuwa kumekuwepo na tuhuma nyingi kutoka kwa mashabiki wa
Madrid na baadhi ya vyombo vya habari nchini Hispania kutoridhishwa na
kiwango cha mwanandinga huyo ikilinganishwa na pesa zilizotumika
kumnunua.
Bale ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa twitter huku
timu hiyo ikitangaza kuachana na kocha wake Carlo Ancelotti.
"nitajituma katika kipindi hiki ambacho msimu umeisha na kutazama mbele
juu ya kurejea tena kwenye msimu ujao nikiwa na nguvu pamoja na Real
Madrid" aliandika Bale. Mchezaji huyo alijiunga na miamba hiyo ya soka
nchini Hispania mwaka 2013 akitokea Tottenham na amekuwa akihusishwa
kurejea tena katika ligi ya England.
No comments:
Post a Comment