
Maafisa wa usalama waaminifu kwa rais wa Burundi Pierre Nkurunzinza wanaendelea na misako dhidi ya watu wanoshukiwa kuwa ''wasaliti'' mjini bujumbura.
BBC ina ushahidi wa uvamizi uliondeshwa na polisi nchini Burundi kufuatia jaribio la mapinduzi ambalo halikufaulu dhidi ya rais Pierre Nkurunziza jumatano iliyopita.
na kufyatua risasi kwenye chumba ambacho wanajeshi na raia waliokuwa wamejeruhiwa katika makabiliano ya siku ya ''Mapinduzi'' walikuwa wakipewa matibabu.
Mfanyikazi mwengine wa hospitali hiyo alisema kuwa wafanyikazi wenzake walishikwa na hofu na wakakimbilia usalama wao.

Mapema ijumaa watu 18 wanaoshukiwa kupanga ''mapinduzi'' hayo, walifikishwa mahakamani lakini kiongozi wao mkuu meja jenerali Godefroid Niyombare hajulikani aliko.
Hapo jana rais Nkurunziza aliwapongeza wanajeshi waaminifu kwa uadilifu wao na ukakamavu uliowawezesha kudhibiti ''wasaliti'' waliokuwa wametangaza ''Mapinduzi'' na kutaka kutibua vita na umwagikaji wa damu nchini humo.

Wakili mmoja aliyekuwa mahakani Anatole Miburo, ameiambia shirika la habari la AFP kuwa walishtakiwa kwa kujaribu kupindua serikali halali.
Bwana Miburo alisema kuwa walikuwa wamepigwa sana hasa Jenerali Ndayirukiye.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Karen Allen amesema kuwa maafisa wa jeshi wanne waliburutwa kutoka hospitalini walipokuwa wakipokea matibabu mmoja wao aliaga dunia.

Wapinzani wake wanadai kuwa Nkurunzinza anakiuka mwafaka wa amani uliowekwa unaomruhusu rais kutawala kwa vipindi viwili pekee.
Watu 25 wamethibitishwa kufariki huku zaidi ya laki moja wakitorokea mataifa jirani wakihofu kutibuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
No comments:
Post a Comment