Serikali ya Ufaransa sasa imemtaka
balozi wa Marekani nchini humo kufika mbele yake kufuatia madai kwamba
Marekani iliwachunguza watangulizi wake wawili.
Mtandao wa
Wikileaks unasema kuwa kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA
kilimpeleleza rais Hollande,Nicholas Sarkozy na Jacques Chiraq kati ya
mwaka 2006-12.
Marais wa Ufaransa
Bwana Hollande ameitisha kikao cha dharura na kusema Ufaransa haitavumilia vitendo ambavyo ni tishio kwa usalama wake. Hatahivyo Marekani imesema kuwa haitatoa tamko kuhusu madai fulani ya kiintelijensia.
Ned
Price ambaye ndio msemaji wa Baraza la kitaifa la usalama nchini
Marekani ameongozea kwamba Marekani hailengi na wala haitalenga
mawasiliano ya Hollande. Wikilieaks
Shirika la NSA lilishtumiwa kwa kumpeleleza kansela wa Ujerumani Angela Merkel pamoja na viongozi wa Brazil na wale wa Mexico.
No comments:
Post a Comment