Kiongozi wa ujasusi wa Rwanda anatarajiwa kufika mahakamani hivi leo kuhusu madai ya uhalifu wa kivita yanayomkabili.
Luteni jenerali Karenzi Karake alizuiliwa katika uwanja wa ndege wa Heathrow Jumamosi chini ya kibali cha kukamatwa cha ulaya.
Rwanda imeonyesha masikitiko yake na kukamatwa kwake.


Miongoni mwa wanaodaiwa kufariki kutokana na matukio hayo ni raia watatu wa Uhispania waliokuwa wakifanya kazi ya kutoa misaada ya kibinadamu katika eneo hilo la kazkazini mwa Rwanda.


Rwanda imekuwa ikishtumu hatua hiyo ya jaji Merelles na kusema ni kutumiwa vibaya na mahasimu wa serikali wenye misimamo mikali na kwamba
jaji huyo hajachukua hatua zipasavyo kupata mashahidi kutoka Rwanda au hata kufanya kazi pamoja na mahakama za Rwanda.
No comments:
Post a Comment