
Rais Omar al Bashir wa Sudan ameondoka nchini Afrika Kusini.
Mwandishi wa BBC aliyeko Afrika Kusini Nomsa Maseko, anasema kuwa ndege ya rais al Bashir ilijazwa mafuta jana usiku na kuwekwa mstari wa mbele tayari kabisa kuondoka katika uwanja wa ndege wa kijeshi.

Mahakama hiyo ilikuwa inapaswa kuamua ikiwa Bwana al-Bashir atakabidhiwa kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ICC yenye makao yake mjini Hague Uholanzi ilikukabiliana na mashtaka ya uhalifu wa kivita na mauaji yahalaiki yanayomkabili .
Majaji watatu walikuwa wanasikiza kesi hiyo rais Bashir alipopuzilia mbali amri hiyo na kuondoka.

Waziri wa mambo ya nje wa Sudan, Ibrahim al-Ghandour, amesema Bwana al-Bashir atarejea Sudan baada ya mkutano huo.
"Tupo hapa kama wageni waalikwa na serikali ya Afrika Kusini.

''Naweza kuwaambia waziwazi kuwa Rais Bashir ataondoka kwa wakati kama ilivyokuwa imepangwa." anasema waziri huyo wa mambo ya nje wa Sudan.
No comments:
Post a Comment