Serikali ya Burundi imekariri kuwa
rais Pierre Nkurunziza hatajiondoa kutoka kinyanganyiro cha urais licha
ya nchi hiyo kukabiliwa na wimbi la maandamano.
Rais Nkurunziza kwa upande wake anashikilia kukutu kuwa ana haki ya kuwania muhula wa tatu kwani muhula wa kwanza alichaguliwa na wawakilishi na wabunge wala sio raia kuambatana na mapatano ya amani.
Msemaji wa rais Philippe Nzobo-nariba amesema swala la rais Nkurunziza kuwania muhula mwengine si la kujadiliwa na kwamba tarehe ya uchaguzi haitaahirishwa tena.
Awali vyama vya upinzani vilikuwa vimepinga ratiba mpya ya uchaguzi iliyotolewa na tume huru ya uchaguzi nchini humo wakihoji uhalali wa ratiba hiyo inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha majuma mawili yajayo.

Kamishna huyo wa kitengo cha umoja wa mataifa kinachohusika na haki za kibinadamu, Zeid Ra'ad Al Hussein amesema wanamgambo hao wanaoiuunga mkono serikali wametuhumiwa kuhusika katika vitendo vya mauji , kuwapiga na kuwanyanyasa baadhi ya wapinzani na kuitaka serikali kukemea na kukomesha vitendo hivyo.
Kitengo hicho cha umoja wa mataifa chasema kimekuwa kikipokea simu kutoka pande mbalimbali za Burundi kulalamikia vitendo kama hivyo na hasa kutishwa na wanaosemekana kuwa wafuasi wa kundi hilo linalojiita Imbone-rakure.
Umoja huo unasema vitendo vya kundi hilo vinazidi kuhatarasha usalama na iwapo vitaendelea vitalipeleka pabaya taifa hilo .
Kwa upande wao serikali imekana kulihami kundi hilo na kuongeza kuwa Burundi ina utulivu wa kutosha kuweza kuendelea na uchaguzi wake.
No comments:
Post a Comment